Ndoa (feat. Khadija Kopa, Juma Kakere & Malkia Karen)

Bright Tanzania

Letra

    Wanangu vipi baba, mbona kimya baba
    Uliahidi jambo, mbona kimya baba
    Mambo ya ndoa umefikia wapi baba
    Mambo yako ya ndoa umekwama wapi niambie

    Nimezunguka dunia mzima
    Dunia kiganja baba, nimeyaona mengi
    Ya walimwengu wanasema
    Bora uchague mpenzi, tofauti na enzi

    Wanafanana kwa sura matendo baba niko hoi eeh
    Unayempenda na kumwaza anamwaza meingine
    Bila pesa umaarufu mwonekano baba we hung'oi eeh
    Na kwa dunia ya sasa, nioe wapi pengine

    Dunia hadaa hilo baba utambue
    Muda unaenda hilo uzingatie
    Mweke Maulana mbele mambo yatimie
    Dhamira yako ya kweli, nayo ajalie

    Baba ooh baba ooh, daddy ooh (baba)
    Najua una hamu sana (mwana)
    Ndoa ooh, ndoa ooh, ndoa ooh
    Ya mi mwanao kuiona
    Kaza roho, kaza roho, dua njema
    Atajibu Maulana
    Mke mwema aah
    Atakuja tu baba

    Ayee (ayee)
    Ndoa eeh (nuia baba)
    Sijamuona wa kuoa eeeh (utaoa mwanangu)
    Ayee (ooh ayee)
    Ndoa eeh (nuia baba)
    Sijamuona wa kuoa eeeh

    Ng'aa tena dafaradhi
    Kumhalalisha mwanangu
    Kwangu mimi ni heshima
    Nikimwona mkwe wangu
    Kudanga danga si kwema
    Kwa leta laana mwanangu
    Leo Ali kesho Juma
    Hebu tuzao twangu

    Mama wakitongoza wanataka kuvua na nguo
    Ah tumejuana leo, anataka kunivua nguo eeh
    Wanaume wa sasa, suruali kushuka eeh
    Mama niombee kwa Mungu
    Nipate mwema niweze sitirika

    Leta mjukuu nimwoe, aje anikojolee
    Ooh, ooh

    Mama ooh, mama ooh, mama ooh
    Najua una hamu sana
    Ndoa ooh, ndoa oooh, ndoa oooh
    Ya mi mwanao kuiona
    Kaza roho, kaza roho dua njema
    Atajibu Maulana
    Mume mwema aaah
    Atakuja tu mama

    Ayee, ndoa eeh (nuia mwana aah)
    Sijamuona wa kunioa eeh (ooh nuia mwana aah)
    Ayee, ndoa eeh
    Sijamuona wa kunioa (sijamuona wa kunioa eeh)
    I say mama ma, mama, mama
    Ayee, ndoa eeh
    Sijamuona wa kunioa (sijamuona wa kunioa eeh)

    Utampata baba ano kuridhia
    Nataka nicheze eeh, mwanangu
    Siku hiyo wanione eeh, mwanangu eeh
    Nikate, nikate, kwa furaha yangu wee eeh


    Comentarios

    Envía preguntas, explicaciones y curiosidades sobre la letra

    0 / 500

    Forma parte  de esta comunidad 

    Haz preguntas sobre idiomas, interactúa con más fans de Bright Tanzania y explora más allá de las letras.

    Conoce a Letras Academy

    ¿Enviar a la central de preguntas?

    Tus preguntas podrán ser contestadas por profesores y alumnos de la plataforma.

    Comprende mejor con esta clase:

    0 / 500

    Opciones de selección