Wandoto

Ibraah

Letra

    Nahisi kama naota
    Na kumbe reality tayari
    Aliyefanya nateseka
    Ni wewe

    Na nafsi inachochota
    Najipa imani sijafeli
    Nahitaji faraja
    Hata chembe nipewe maa

    Macho pembeni nisikupe pesa
    Kwako yaani nishafika
    Kumbe makucha uliyaficha
    Na ushanikwarua ooh

    Na zangu hisia umeziteka
    Nilipokosea sawazisha
    Usije hadharani kuanika
    Ukaniumbua oh nah, nah, nah

    Na nakuombea Mungu
    Akuepushe na mabaya
    Hali dhiki mafungu
    Ila la kwangu ndo limepwaya

    Nalia nalia kwa uchungu
    Umenitoroka nyuma ya idhaya
    Ni wewe japo nilikudhamini
    Na nikakuitaga

    Wandoto wandoto
    Wandoto, wandoto
    Ah ni wewe wa ndoto
    Leo penzi umeliweka vikwanzo

    Wandoto wandoto
    Wandoto, wandoto
    Wandoto uliyekuwa ni wewe
    Na kichwa umekiachia mawazo

    (Ooh, ooh, aah yeiye)

    Kweli usiku wa giza usilolijua
    Sikuwaza, sikudhania kuwa utanibagua
    Sa unafikiri nani wa kupika pakua
    Ni wewe

    Kishida kijiba cha roho mwenzako naugua
    Haya no commando siwezi jipindua
    Nawe ndo dereva umezamisha mashua
    Ni wewe ni we eh

    Ila mwenzako bado bado
    Moyo unasonona
    Manati bila kipago
    Nikuulize wapi uliona

    Mi nina uzoefu wa kufunga goal
    Uvivu wa kufua foronya
    Yaani siamini yes umegeuza no
    Na kwako mi mtoto nahitaji nyonya

    Wandoto wandoto (ni wewe)
    Wandoto, wandoto
    Ah ni wewe wa ndoto
    Leo penzi umeliweka vikwanzo

    Wandoto wandoto
    Wandoto, wandoto


    Comentarios

    Envía preguntas, explicaciones y curiosidades sobre la letra

    0 / 500

    Forma parte  de esta comunidad 

    Haz preguntas sobre idiomas, interactúa con más fans de Ibraah y explora más allá de las letras.

    Conoce a Letras Academy

    ¿Enviar a la central de preguntas?

    Tus preguntas podrán ser contestadas por profesores y alumnos de la plataforma.

    Comprende mejor con esta clase:

    0 / 500

    Opciones de selección