visualizaciones de letras 4

Sudi Sudini

Isha Mashauzi

Letra

    Mja hapati, hapati alitakalo
    Bali hupata, ajaliwalo na Mungu
    Usikonde, kwa hili nilipatalo
    Hilo ndilo, hilo ndilo langu fuu

    Mja hapati, hapati alitakalo
    Bali hupata, ajaliwalo na Mungu
    Usikonde, kwa hili nilipatalo
    Hilo ndilo, hilo ndilo langu fuu

    Sudi, sudi sudini
    Bahati ya mwenzio, usilale mlango wazi
    Sudi, sudi sudini
    Bahati ya mwenzio, usilale mlango wazi

    Ni lipi nililowakosea?
    Mbona yenyu ni machafu hamsemi
    Mabaya, kutwa kunipakazia
    Kama nina deni niambieni

    Maana kila siku maneno
    Mie si mtu, hilo linatoka wapi?
    Mmenibadilisha jina naitwa mchawi
    Tena hasidi, yote yanatoka wapi

    Maana kila siku maneno
    Mie si mtu, hilo linatoka wapi?
    Mmenibadilisha jina naitwa mchawi
    Tena hasidi, yote yanatoka wapi?

    Niliyajua mapema ndo maana nikapuuzia
    Washa zoea kusengenya ndo maana nawapotezeaga
    Si hofii mi wenu unafiki, shingoni sijitii kamba
    Wajidanganya na vyenyu visiki, sumu yenyu sitoilamba
    Alopewa na Mola hapokonyeki, wala msijisumbuke kwa dumba
    Wajidanganya na vyenyu visiki, sumu yenyu sitoilamba

    Mwanitangazia, mwajitangaza mitaani
    Kwamba mnanijua, mimi kiundani wewe
    Kuliko hata alonileta duniani wewe

    Tena mnajinadi, huko mitaani wewe
    Kwamba mnanijua, mimi kiundani wewe
    Kuliko hata alonileta duniani wewe

    Nyie kama mahodari basi naye mseme
    Yaani nyie kibindoni wana wa wezenu midomoni
    Nyie kama mahodari basi naye mseme
    Yaani nyie kibindoni wana wa wezenu midomoni

    Sudi sudini, asiye bahati habahatishi
    Sudi nichukie nyinyi, tamaa hamnikatishi
    Mwajipatia dhambi nyinyi, nalala mie sikeshi

    Ikiwa kuna kuozwa nahisi nimetenda
    Basi niko radhi chini niweke mimi
    Kuliko kukaa pembeni, mabaya kuzua
    Na mimi nina roho, kama nyinyi

    Hata ukiwa mwerevu wao watakugeuza ng'ombe
    Kusudi wakupake majivu, hao hawana aibu viumbe
    Nafeli kwa kukosa usikivu, hamna subira hata chembe
    Mnapoteza mwenzenu kwa mambo yenu ya kizembee

    Sibabaiki na yenu majungu mie
    Mie nawaua kisugu mie
    Mwasaka kiti kupitia jina langu
    Ukimya ndo sina haya hangu mie
    Mmesahau kuwa kuna Mungu
    Mwapinga ramli chini ya uvungu nyie

    Sudi sudini, asiye bahati habahatishi
    Sudi nichukie nyinyi, tamaa hamnikatishi
    Mwajipatia dhambi nyinyi, nalala mie sikeshi

    Sudi sudini, asiye bahati habahatishi
    Sudi nichukie nyinyi, tamaa hamnikatishi
    Mwajipatia dhambi bure, nalala mie sikeshi

    Pole, pole sana eeh
    Pole, pole sana eeh
    Na kila kitu mimi
    Mimi mchawi wako mimi
    Mimi hasidi yako mimi
    Mimi na ubaya wako mimi
    Kila kitu mimi

    Pole, pole sana eeh
    Pole, pole sana eeh
    Umeshinda ugangani, kesha uchawini
    Sina hirizi shingoni, shina ushale mwilini
    Mimi najiamini, namtegemea maanani

    Pole, pole sana eeh
    Pole, pole sana eeh
    Na kila kitu mimi
    Mimi mchawi wako mimi
    Mimi hasidi yako mimi
    Mimi na ubaya wako mimi
    Kila kitu mimi

    Pole, pole sana eeh
    Pole, pole sana eeh

    Kuna nazi, kuna nazi
    Kuna nazi, haya kuna nazi
    Kukuna nazi kwahitaji ujuzi wewe
    Kama hujui nenda muulize somo yako
    Kukuna nazi kwahitaji ujuzi wewe
    Kama hujui kamuulize somo yako wee

    Mi mwenzangu anakuna nazi, haya kuna nazi
    Haya imba mwenzangu anakuna nazi, haya kuna nazi
    Nazi kweli jamani inampendwa wewe
    Ila kukuna eeh yahitaji ujuzi wee
    Na iwapo wataka kujaribu wewe
    Basi nenda uulize wenye ujuzi wee
    Angalia usilete upuzi wewe
    Kukuna nazi kwahitaji ujuzi wee

    Mi mwenzangu ana-kuna nazi, haya kuna nazi
    Haya sasa mimi na kuna nazi, haya kuna nazi

    Kukuna nazi kwahitaji ujuzi wewe
    Kama hujui nenda muulize somo yako wee
    Mi mwenzangu ana-kuna nazi, haya kuna nazi
    Mi hodari kukuna ee kuna nazi, haya kuna nazi
    Haya imba mwenzangu ana-kuna nazi, haya kuna nazi

    Sitaki, sipendi, naogopa
    Anajijua yeye kwamba yeye si mzima
    Anataka kumpa mwenzake maradhi
    Anajijua yeye kwamba yeye si mzima
    Anataka kumpa mwenzake maradhi
    Kwa makusudi

    Sitaki, sipendi, naogopa, sitaki
    Anajijua yeye kwamba yeye si mzima
    Anataka kumpa mwenzake maradhi
    Anajijua yeye kwamba yeye si mzima
    Anataka kumpa mwenzake maradhi
    Kwa makusudi

    Sitaki, sipendi, naogopa, sitaki

    Umelikoroga hilo, leo utalinywa hilo
    Umelikoroga hilo, leo utalinywa hilo
    Umelikoroga hilo, leo utalinywa hilo

    Maneno ya watu wanapenda uwongo (hicho kiranga)
    Ua fisi wapi? Kutwa kimbelembele (hicho kiranga)
    Watu washamjua pembeni wanamcheka oooh

    Umelikoroga hilo, leo utalinywa hilo
    Umelikoroga hilo, leo utalinywa hilo

    Ugomvi si wake kutwa kimbelembele (hicho kiranga)
    Kuchukia watoto wa wenzake bila sababu (hicho kiranga)
    Kuingililia maneno yasiyo mhusu (hicho kiranga)
    Wenzake washamjua pembeni wanamcheka

    Umelikoroga hilo, leo utalinywa hilo
    Umelikoroga hilo, leo utalinywa hilo
    Umelikoroga hilo, leo utalinywa hilo

    Chachizi ukimpa tatizi alitatue ni tatizi (haha)


    Comentarios

    Envía preguntas, explicaciones y curiosidades sobre la letra

    0 / 500

    Forma parte  de esta comunidad 

    Haz preguntas sobre idiomas, interactúa con más fans de Isha Mashauzi y explora más allá de las letras.

    Conoce a Letras Academy

    ¿Enviar a la central de preguntas?

    Tus preguntas podrán ser contestadas por profesores y alumnos de la plataforma.

    Comprende mejor con esta clase:

    0 / 500

    Opciones de selección