visualizaciones de letras 3

Nisamehe (feat. Aslay)

Kala Jeremiah

Letra

    Nakiri nilikuumiza sana mama yangu
    Nyumbani kukugonganisha na machangu
    Pia kukugombanisha na ndugu zangu
    Ili mradi nifurahi ndani ya nafsi yangu
    Nakunywa ninalewa na rafiki zangu
    Nakuangushia kipigo na una mimba yangu
    Mpaka mimba ikachoroboka kwa ujinga wangu
    Leo nitaficha wapi mimi sura yangu?
    Mbele sioni kitu zaidi ya ukungu
    Na maadui wako wengi zaidi ya nywele zangu
    Nishike mkono mikosi inaniandama
    Na usipo nionea huruma haki ya nani nitazama
    Mwili hauna nguvu kama mwenye homa
    Nahisi niko kuzimu na shetani ananichoma
    Ongea chochote na nafsi yangu itapona
    Nakiri sitorudia tena mbele ya Maulana

    Najua unanisikiaaa
    Ila kunijibu ndo huwezi
    Eeeh Mungu baba saidiaaa
    Umlaze mahala pema mpenzi
    Na pia anisamehe maha, anisamehe
    Na pia anisamehe sana, anisamehe

    Nisamehe nitakufa, kwa mawazo ya msongo
    Wapambe walionipamba, wamenigeuzia mgongo
    Baada ya kuishiwa pesa, wanadai sina mpango
    Ni kweli sina dini, wala sina mchongo
    Siku hizi sinywi bia, ni viroba mixer gongo
    Nisikufiche, nimepoteza malengo
    Kwenye kupa kwa mizigo, kwenye lori mi ndio tingo
    Maisha yangu yanaelekea ukingo
    Na kama nitakufa leo, jua kuu uliacha pengo
    Nikiongea sana nikajitukana
    Maana nilifungwa macho na starehe za ujana
    Nikajiita pimpi kicheche bonge la bana
    Nikakupa mateso ya moyo, mwili kimwana
    Na kila nilipolewa ni kichapo cha kufana
    Nishike mkono japo nimelewa sana
    Sema neno moja liuponye mwili wenye laana

    Najua unanisikiaaa
    Ila kunijibu ndo huwezi
    Eeeh Mungu baba saidiaaa
    Umlaze mahala pema mpenzi
    Na pia anisamehe maha, anisamehe
    Na pia anisamehe sana, anisamehe

    Nakiri sina uti, ila sasa nakwangukia
    Unanijua vizuri, sina haja ya kuhadithia
    Ila sirudii makosa haki ya Mungu naapia
    Sauti za kuzimu ninazisikia
    Bila msamaha wako hakika nita disappear
    Mi kipofu niongoze, natanga sioni njia
    Nakiri mi ni bonge la fala tena mburula
    Nilikuona taka-taka nikazurura
    Nikapiga chaka kwa chaka na kina Shura
    Sasa cheki nilivyo, nimenyooka kama rula
    Natamani ardhi ipasuke nijifiche sura
    Ama kweli dunia imenielemea
    Mzigo ni mzito Golgotha naelekea
    Ndugu wa damu yangu, sioni walikoelekea
    Hakika ni wewe pekee unaweza kunitetea
    Nadhani sasa sina tena cha kuongea

    Najua unanisikiaaa
    Ila kunijibu ndo huwezi
    Eeeh Mungu baba saidiaaa
    Umlaze mahala pema mpenzi
    Na pia anisamehe maha, anisamehe
    Na pia anisamehe sana, anisamehe


    Comentarios

    Envía preguntas, explicaciones y curiosidades sobre la letra

    0 / 500

    Forma parte  de esta comunidad 

    Haz preguntas sobre idiomas, interactúa con más fans de Kala Jeremiah y explora más allá de las letras.

    Conoce a Letras Academy

    ¿Enviar a la central de preguntas?

    Tus preguntas podrán ser contestadas por profesores y alumnos de la plataforma.

    Comprende mejor con esta clase:

    0 / 500

    Opciones de selección