Suscríbete

Ndoto Ya Mchana

Leteipa the King

Letra

    Niliskia tufununu, Kwamba ulipata mwingine
    Anayekupenda zaidi ya mimi, mtafunga ndoa pengine
    Yetu ilikuwa shadow, mapenzi yenu yamekolea
    Lazima huwa Anakupa, vitu sikuwa nakupea
    Ndoto zako zote, ulizoniambia
    Naona kama kweli sasa zinatimia
    Na Sina chochote, cha kukuambia
    Ila nakonda Kweli nikikufikiria

    Sura yako umbo lako jamani eeh
    Busu na mahaba chumbani maami
    Mawaidha yako nikiwa matatani eeh
    Nikikumbuka najiona hayawani maami

    Nawatakia mema (nawatakia mema)
    Nawatakia mema (nawatakia mema)
    Nawatakia mema (nawatakia mema)
    Basi kwaheri kwaheri kwaheri Mami (ndoto yangu ya Mchana)

    Ingawa inaniuma, niko na furaha moyoni
    Kuona kwamba umepata, vyote ulivyokuwa unatamani
    Naomba nipate mwaliko, wa harusi nije Nile wali
    Nipige picha na wadau, nikupe zawadi kama zamani
    Alafu ntapeform, kama beshte yako, kale kawimbo nilikuimbia shambani
    Na nitakuinform, tunza mume wako, Japo kuna vitu zenye ninatamani

    Ingawa ningependa, ungekuwa wangu pekee (nawatakia mema)
    Ingawa moyoni umeniachia kidonda (nawatakia mema)
    Namwomba Mungu, anipatie mwingine Kama wewe (nawatakia mema)
    Hivo kwaheri kwaheri kwaheri kwaheri mama (ndoto yangu ya Mchana)
    Lakini ninaomba, unifanyie favour Moja (nawatakia mema)
    Ukijifungua kama ni wa kiume, mpe jina laangu (nawatakia mema)
    Na kama ni wa kike mpe jina la mama yangu (nawatakia mema)
    Basi kwaherii (ndoto yangu ya Mchana)


    Comentarios

    Envía preguntas, explicaciones y curiosidades sobre la letra

    0 / 500

    Forma parte  de esta comunidad 

    Haz preguntas sobre idiomas, interactúa con más fans de Leteipa the King y explora más allá de las letras.

    Conoce a Letras Academy

    ¿Enviar a la central de preguntas?

    Tus preguntas podrán ser contestadas por profesores y alumnos de la plataforma.

    Comprende mejor con esta clase:

    0 / 500

    Opciones de selección