Bomba Ipepee (feat. Stamina & Mr. Blue)

Manengo

Letra

    Here's another one!

    Na nisipotoka sio tu Mungu mpaka shetani ata doubt
    Warrup, tumia akili kabla haijakutumia
    Manengo, you know me (touch!)
    Stamina, you know me
    Busy, busy, busy, let's go!

    Okey, niko peke yangu, sina dada wala ndugu
    Wakinitaka nipo baa nakunywa Pombe Magufuli
    Gigi kunipa papa, mliona wivu ka napanda ndwafu
    Waambieni nipo Kenya napewa Papa Jones na Khaligraph
    Waambieni watoto warudi shule
    Nawashangaa wanauza K wakati Mwanza zihuwa bure
    Saa, kanikimbia Mwanza kaenda Tambora kaliwa
    Chungeni msicheze Iokote gerezani mtalia
    Mi ni Yanga, nampiga mdogo na mkubwa yaani
    Namkalisha danda mpaka simba wa Yuda
    Similiki dem, similiki shem
    So ukiniona ninajichua jua nina maumivu sehem
    Picha ya Mjoni, so hamjui ata kusoma
    Kwa manengo wamecheka na mla mhindi wa kuchoma
    Na sio Bongo tu, nenda Mozambique watakwambia kuwa
    Nauza chai ya rangi, ubongo maziwa

    Kama jahazi linasonga
    Wacha bomba ipepee, wacha bomba ipepee
    Mpaka tuna tia nanga
    Wacha bomba ipepee, wacha bomba ipepee

    Watoto wamejiroga
    Kimya na kuguza guza soda
    Watu wazima cheki tunavuka boda
    (Watu wazima cheki tunavuka boda)

    Ah, na huu mwaka nawachezesha kichura chura
    Kikuta napiga tano, cargonini huko manura
    Pole mnafiki Mr Yuda, mbele yangu huwezi tamba
    Naona unapoteza muda ka mshenga wa Dogo Njanja
    Wanaonijua vizuri hawana shaka na mimi
    Wanadata na mimi, nikitema wanadaka madini
    Mtu makini, mchezoni mi huuza sura kwa nini?
    Ngumu kumeza, Mr Paka roho saba kazini
    Ukiona anatingisha kichwa, cheki na zipu
    Maana nina vichwa viwili navyo tumia kila siku
    Waambieni wapizani, habari yao tunayo
    Wasije CCM kirhumba, watapigwa roba za mbao
    Shoga ukikosa vumba, danga
    Kuhusu bikogo ya mapenzi pata mchumba, Tanga
    Ah kula sana unga, wanga
    Ukipata dem kisu tafta chumba, manga

    Kama jahazi linasonga
    Wacha bomba ipepee, wacha bomba ipepee
    Mpaka tuna tia nanga
    Wacha bomba ipepee, wacha bomba ipepee

    Watoto wamejiroga
    Kimya na kuguza guza soda
    Watu wazima cheki tunavuka boda
    Watu wazima cheki tunavuka boda

    Nina mistari nidhamu, tega sikio niwaonyeshe
    Yaani mi ni mtamu, mpaka Nandy aliniomba nimnogeshe
    Manengo ni chuo bro na sio veta
    Napigaga guitar, kinanda hadi zezeta
    Waambieni watabiri wa ndoto, mi hizi ndoto zinanionea
    Maana nikilala na mto huwa naotaga naogelea
    Na ununda wangu wote, sijawai kwenda segerea
    Ghetto navuta subira, kuliko powder na mmea
    Mi nimeshazoea ng'ombe na mbuzi nusu
    Kwa hiyo siridhishwi na dem mwenye kikuku
    Msichojua, kwenye collabo, namkalisha mkali wao
    Mkuje simba, paka na mkali wenyu
    Kuhustle ndo kauli mbiu, amkeni washikaji
    Unaeza ukafa na kiu na huku unakaa ubongo maji
    Nilikotoka ni hatari, hakiombeki hali mbaya
    Hata nikifa bila gari, nitaendesha huko Galilaya

    Kama jahazi linasonga
    Wacha bomba ipepee, wacha bomba ipepee
    Mpaka tuna tia nanga
    Wacha bomba ipepee, wacha bomba ipepee

    Watoto wamejiroga
    Kimya na kuguza guza soda
    Watu wazima cheki tunavuka boda
    Watu wazima cheki tunavuka boda

    Lazima cheki tunavuka boda
    Bomba ipepee, acha bomba ipepee
    Ooh wooh, acha bomba, acha bomba (touch!)
    Tumia akili kabla haijakutumia


    Comentarios

    Envía preguntas, explicaciones y curiosidades sobre la letra

    0 / 500

    Forma parte  de esta comunidad 

    Haz preguntas sobre idiomas, interactúa con más fans de Manengo y explora más allá de las letras.

    Conoce a Letras Academy

    ¿Enviar a la central de preguntas?

    Tus preguntas podrán ser contestadas por profesores y alumnos de la plataforma.

    Comprende mejor con esta clase:

    0 / 500

    Opciones de selección