visualizaciones de letras 78
Letra

    Wewe ndiwe Baba
    Wewe ndiwe Mungu
    Wewe ndiwe Baba
    Usikie kilio chao

    Wengine walia mavazi
    Wengine walia chakula
    Wengine walia kulala
    Wengine walia msaada

    Wasaidie
    Eh he, Wasaidie
    Oh, Wasaidie
    Eh, Wasaidie

    Enyi wazazi wa kambo
    Msiwatese yatima
    Enyi wazazi wa kambo
    Msiwatese yatima
    Nao ni watu, mbele za Mungu
    Tena wana haki, mbele za Mungu
    Msiwatese!

    Wanalia, ye ye ye
    Eh Mungu, sikia kilio chao!
    Hawana baba wala mama
    Ee Bwana, wasaidie
    Wewe ndiwe msaada wao
    Ee Bwana, wasaidie

    Wameumizwa sana na maneno ya watu
    Wameumizwa sana na maneno ya Walimwengu
    Ondoa
    Ondoa uchungu mioyoni mwao
    Ondoa mawazo mioyoni mwao
    Ondoa mikwasi mioyoni mwao
    Ondoa hasira mioyoni mwao

    Walikula vizuri
    Leo wala majalalani
    Walilala pazuri
    Leo walala mitaroni

    Mali zao mmechukua ninyi ndugu zao
    Wakija kuomba chakula, mwawanyima
    Wakija kuomba
    Mwawafukuza kama mbwa

    Kuna siku, watoto
    Wenu wataitwa yatima
    Na watateswa kama mlivyowatesa
    Ee Mungu, watazame yatima
    Watie nguvu, wasikate tamaa

    Kuna siku, watoto wenu wataitwa yatima
    Na watateswa kama mlivyowatesa
    Wanalia, ye ye ye
    Eh Mungu, sikia kilio chao!

    Yesu, naomba unitazame mimi yatima
    Maana mama ameniacha
    Walikuwepo nilidhamimiwa sana
    Lakini kwa sasa, dhamani yangu haipo tena
    Nisaidie, ewe Yesu

    Tunapokwenda, wewe ndiwe kimbilio
    Kwanini mimi, kwanini mimi niitwe yatima?


    Comentarios

    Envía preguntas, explicaciones y curiosidades sobre la letra

    0 / 500

    Forma parte  de esta comunidad 

    Haz preguntas sobre idiomas, interactúa con más fans de Mtukizeni Chior y explora más allá de las letras.

    Conoce a Letras Academy

    ¿Enviar a la central de preguntas?

    Tus preguntas podrán ser contestadas por profesores y alumnos de la plataforma.

    Comprende mejor con esta clase:

    0 / 500

    Opciones de selección