Kaka Tuchati

Rostam Tanzania

Letra

    (Tongwe Records)

    Ooii naona mtandao unakatika
    Upo kimya sana mkato au kunde imevunjika
    Na mtanyooka roundi hii
    Na hivi huwezi bila mimi?

    Najikuta Jay Z oya unarudi lini?
    Kaka huku wamefunga mipaka
    Ila tiketi nilikata nirudi kabla ya pasaka
    Rudi ugeuze kisu sio
    Mwana wa kulitafuta mwana wa kulipata
    Round hii sio nunio, daraja la mpasu

    Kumekucha hivi saa ngapi huko nipe takwimu
    Nimeamka nishaweka bundle namngoja Umi mwalimu
    Anapambana yule dada
    Tanga nimewavulia kofia wametoa sanitizer za iliki
    Yaani ukipaka unanukia

    Hehehe Corona nishai yaani Bongo kila mtu daktari
    Masai kachemsha maji ya mpapai kanywa na sukari
    Guza hadi maski wanafua sijui ni nani kawafundisha
    Huku kuna dada kajifukiza mashetani kayapandisha

    Tueke siasa kando unajua uchumi unashuka
    Sio Bongo tu hadi ng'ambo watu wamefunga maduka
    Hapa nawaza pesa ya bango benki walokopa wanajuta
    Tukisema tukae ndani na hii njaa si tutakufa

    Hali inatisha na umasikini, tunaoumia ni sisi
    Yaani bora ufe kwa Ukimwi angalau utaandika urithi
    Kwa iyo hamna bata, sio kidimbwi sio tipsi
    Kaka madanga yamekata so hazitimbi hizo piece

    Bwana wa mabwana Mungu wa miungu
    Alpha na Omega nani kama wewe
    Bwana wa mabwana Mungu wa miungu
    Alpha na Omega nani kama wewe

    Hivi unakaa jimbo gani au Marekani
    Unajikinga vipi maana vifo vingi hadi siamini (Mmmh)
    Au umesharudi ipo zako Horohoro nini
    We bwana hebu niache mi nimeze chloroquine

    Umenikumbusha kweli Chloroquine ni dawa?
    Bado inafanyiwa uchunguzi ila haijadhibitishwa
    Ingawa ukinywa haitohatarisha ndio maana bado wanaigawa
    Mi ninakunywa maana nilishika uso kabla ya kunawa

    Eti unaweza ukawa nayo na usionyeshe dalili?
    Ewaah! Uko sahihi, na kingine kuhusu hili ni kwamba
    Mgonjwa wa Corona unaweza usimtambue kwa macho
    So mtu yeyote unayemuona mpe mita mbili toka kwako

    Na hiko kiVansileka ndo kinini baba wawili?
    Ni ventilator, ni mashine ka mapafu ya nje ya mwili
    Mmmh sijaelewa hebu nieleweshe kuhusu hili
    Naskia vinauzwa ghali basi viwe vingi Muhimbili

    Okay, kirusi cha Corona kinashambulia mapafu
    Ndipo zinaanza homa, kifua alafu
    Unashindwa kupumua na mwili unahitaji tafu
    Ventilator huingiza hewa na kuitoa iliyo chafu

    Tuepuke mikusanyiko ikibidi tukae ndani
    Tumeambiwa tujifukize hivi ni dawa unadhani?
    Ngoja kwanza, hivi fumigation (Mmmmh mmh)
    Baba ile inaua mende eti (Hahaha wacha utani)

    Bwana wa mabwana Mungu wa miungu
    Alpha na Omega nani kama wewe
    Bwana wa mabwana Mungu wa miungu
    Alpha na Omega nani kama wewe

    Maisha ya upweke yanasumbua ila siku zinapita
    Yule mkewe itunze pete
    Mtayamaliza na uhakika kaka
    Ila hatua dua haina haja ya kusikitika

    Ila navyokujua hujazini miezi sita?
    Kiukweli mi mwaminifu ingawa jogoo anawika
    Mama Ivan mbabaifu haku-cheat una uhakika?
    Kuna mchezaji wa Yanga namwona anapita pita

    Nitamkata kata mapanga yaani namuua na namzika
    Oyaah wape nyumbani basi pesa ya matumizi
    Kaka nitoe wapi na show hakuna siku hizi?
    Hali imekuwa ngumu hakuna pesa kila kona

    Kila mtu unayemdai naye anasingizia Corona
    Mbona sasa wanafunga shule na vyuo alafu bar hawafungi
    Mzazi atamlindaja mtoto na akirudi yuko tungu?
    Polisi India wanapiga watu wakisongamana

    Wao barakoa hawana, jua defender wamebanana
    Sasa wanatukusanya kutuambia tusikusanyike
    Ila wauguzi wanajitoa sana, dah Mungu awalipe
    Wapinzani mnatangaza vifo walopona hamwatangazi

    Ah-ah wanasema wangeweka takwimu za wazi ingekuwa kizazi
    Kwa hivyo lockdown hakuna alafu umeona text niliyotuma?
    Ipi kwenye group mbona inbox hakuna?
    Ah naskia (Nini?) koyuzeka mbochi
    Maana uliko uliko usiongee sana inatosha
    Hadi papai lina Corona dah (Kaka tuchati)
    Mmmh ina mbuzi vipi? (Eeh eh kaka tuchati)
    Mwili umekufa ngazi (Kaka tuchati)
    Poa mwanangu tuendelee kujifukiza

    (Tongwe Records, Bin Laden)


    Comentarios

    Envía preguntas, explicaciones y curiosidades sobre la letra

    0 / 500

    Forma parte  de esta comunidad 

    Haz preguntas sobre idiomas, interactúa con más fans de Rostam Tanzania y explora más allá de las letras.

    Conoce a Letras Academy

    ¿Enviar a la central de preguntas?

    Tus preguntas podrán ser contestadas por profesores y alumnos de la plataforma.

    Comprende mejor con esta clase:

    0 / 500

    Opciones de selección