Kijiwe Nongwa

Rostam Tanzania

Letra

    Alikuja kama masii tukamchangia sadaka
    Tukamwona nabii aliyeshushwa siku ya pasaka
    Tukamtolea na zaka ili kanisa lijengwe
    Eeh-eh na bado wakamlaza nabii kifo cha mende

    Hivi unamkumbuka babu? Babu wa Loliondo
    Ah-ah yule mfugaji mwenye bleach la kikogo
    Watu wamekufa, watu wamefungwa, watu wamepoteza biashara
    Sasa umekaribia uchaguzi amerudi chama tawala

    Vipi dada yetu wa Igunga, mmh simwoni udangani
    Ah mbona ashapata mchumba sio viben 10 wa zamani
    Yule fundi gereji chawa, si kamateka bibiye
    Na wamefungua mgahawa, yaani wote mama ntilie

    Na kuna dem aliyeachiwa mtoto akaolewa na mtoto
    Akaachana na mtoto akabaki anamlea mtoto
    Hizi ndoa za mjini bwana, zinasikitisha
    Eeh maana hufungiwa chumbani na huvunjikia Insta

    So soka la Bongo linakwama wapi? TFF maanake nini
    Tanzania Football Failure, ndo nacho jua mimi
    Unamfukuzaje Amunike ili udhaifu wenu umvuge
    Wakati mlimpeleka mlevi ye akacheze namba ya Mkude?

    Nasema leo hakilali kiporo, imeshakuwa kero
    Ukuta tunavunja kwa tindo
    Wameshapigwa guu wako telo
    Na kiki za kikolo
    Majita tushapiga kishindo

    Hili ni fagio la chuma
    Linang'oa visiki
    Safisha vichaka kwa moto
    Simba kageuka duma
    Jangwa halipitiki
    Ukitufuata umetoa boko

    Marehemu walimsema mnyonyaji, kwani mziki una maziwa?
    Sasa Mungu kamhitaji na bado hajafanikiwa
    Hivi unadhani ndani ya mjengo nani ataliziba pengo?
    Acha maisha yaendelee, jasiri ameumaliza mwendo

    Aliyeokota almasi mchangani alikuwa Miss Tanzania
    Na aliyekuja inunua dukani ni Mganda aliyekuwa na nia
    Ya dhati la pakato akatokea mara mia
    Akawatumia ila mwamba ni mnyanyasaji wa kijinsia

    Sa skiza man hii, vipi shem mama Ivan?
    Ah tupo tupo tu ila hatupo ka zamani
    Nawe vipi kwani, mbona wife simuoni nyumbani
    Hey chill man, sina majibu deal done

    Bungeni daily majanga, viongozi wameishiwa mada
    Hivi mbunge wako wa Tanga hoja zake unaziskiaga?
    Sa nitazisikiaje? Na Ana spika mbovu za wana kijiji
    Ila fundi wao anakuja soon kutoka Ubelgiji

    Nabii Tito na Dr Shika, tayari wamesahauliwa
    Mwenzao Mariamu, biriani anapika anapakuliwa
    Bongo bwana, ndo nchi inayosupport sana ujinga
    Utashangaa Amber Rutty kala shavu ubalozi wa kinga

    Yaliyosemwa yamesemwa
    Kazi kwenye mmezoea kutema
    Wakitaka tuyajenge tena
    Waambie muda sio rafiki mwema
    (Yeiye iyee, aah aah iyee)

    Kusema kweli hatuchoki
    Na kwenda jela hatuogopi
    Tutabanana ata kama hapatoshi
    Hatupindishi ata kwa dumba

    Nasema leo hakilali kiporo, imeshakuwa kero
    Ukuta tunavunja kwa tindo
    Wameshapigwa guu wako telo
    Na kiki za kikolo
    Majita tushapiga kishindo

    Hili ni fagio la chuma
    Linang'oa visiki
    Safisha vichaka kwa moto
    Simba kageuka duma
    Jangwa halipitiki
    Ukitufuata we toa boko


    Comentarios

    Envía preguntas, explicaciones y curiosidades sobre la letra

    0 / 500

    Forma parte  de esta comunidad 

    Haz preguntas sobre idiomas, interactúa con más fans de Rostam Tanzania y explora más allá de las letras.

    Conoce a Letras Academy

    ¿Enviar a la central de preguntas?

    Tus preguntas podrán ser contestadas por profesores y alumnos de la plataforma.

    Comprende mejor con esta clase:

    0 / 500

    Opciones de selección