visualizaciones de letras 3

Nimwage Radhi (feat. Harmonize)

Mrisho Mpoto

Letra

    Alilililii
    (Ayo lazer!)

    Furaha isio kifani, kumpata mwandani
    Hakika wamependeza
    Ngoma lipo uwanjani, kaibiwa nani
    Sa unaachaje kucheza

    Hama kweli harusi imefana tena ya kihistoria
    Pande zote, baba na mama, naona wanashangilia
    Ila sitaki kua mnafki, Jumba bovu kuniangukia
    Nina langu la moyoni, ningependa kuwaambia
    Bi harusi, mashoga wakupupia
    Hao niwakuwaangalia
    Wako wale wahali gani, wanakuja kuchungulia
    Uwaombe samahani, uwakomeshe wambea
    Eti, wifi umepika nini, na mimi utanigaia
    Waambie, wamepika p dagaa, zenye pilipili nyingi
    Zakutisha we na mumeo, wao watakimbia

    Aii shemeji
    Ndugu yo mumeo, usisikilize ya fulani
    Na hii ndio meseji
    Sema na mumeo usifuate ya jirani
    Kwa furaha niliyo nayo

    Niacheni nimwage radhi (alilililii)
    Mi nataka nimwage radhi (ai yoi yooo)
    Niacheni nimwage radhi
    Mi nataka nimwage radhi (alilililii)

    Ng'ombe anapoita ndama, tunasema kua analia
    Kupigwa na kulalama, hatujawahi kusikia
    Hakika mmependeza
    Ninavyomfahamu biharusi, sipati kusimulia
    Nimetoka Ruvuma, Mchomori, namtumbo
    Lindi, mtwara mpaka chitohori nimezisikia
    Sifa za binti huyu, Mola amemjalia
    Binti hapendi majungu, hakika ninawaambia
    Ukimuazia viatu na gauni, anakuachia
    Bwana harusi tunakupa mke, ukaishi nae vyema nyumbani
    Huna kitu usimfiche mwambie, taabani
    Ikiwezekana mkakope, mkono uende kinywani
    Usimpige mateke, kisingizio kitu fulani
    Ooh umefanya nini jana, hakuliki leo ndani
    Mtoto bado mteke, usimkomaze Kwa ngumi
    Ukimshindwa mrudishe, kwao hajaua huyu
    Mumeo akienda kazini, akirudi salimia
    Wala usikae chini, chakula kumsukumia
    Bali mkaribishe ndani, hali kumjulia
    Muulize za kazini, kwa tabasamu muruua
    Kisha msindikize bafuni, hata kama anapajua
    Halafu wewe tafuta kiti, jikoni kimbilia
    Chukua simu yako message, ukimtumia
    Mwambie hasilani bila wewe, chakula hakitaingia

    Eh!
    Aii shemeji
    Ndugu yo mumeo, usisikilize ya fulani
    Na hii ndio message
    Sema na mumeo usifate ya jirani
    Kwa furaha niliyo nayo

    Niacheni nimwage radhi (alilililii)
    Mi nataka nimwage radhi
    Niacheni nimwage radhi
    Mi nataka nimwage radhi (alilililii)

    Nawaomba niishie hapa tarishi huwa hafungwi
    Naomba nichape lapa, yaliobaki ni ya makungwi
    Niliowakera samahani kusema ni jukumu langu
    Nawaomba muishi kwa amani hio ndio furaha yangu

    Mmh ndio ni kama safari tuombeane dua
    Atuepushe na shari saa chini ya jua
    Aah somo yake mwari, ainuke
    Mama yake mwari, ainuke
    Baba yake mwari, aunike
    Aje kati tuicheze ngoma
    Aah kaka yake mwari, ainuke
    Dada yake mwari, ainuke
    Shangazi yake mwari, ainuke
    Aje kati tulicheze ngoma

    Niacheni nimwage radhi
    Mi nataka nimwage radhi
    Niacheni nimwage radhi
    Mi nataka nimwage radhi


    Comentarios

    Envía preguntas, explicaciones y curiosidades sobre la letra

    0 / 500

    Forma parte  de esta comunidad 

    Haz preguntas sobre idiomas, interactúa con más fans de Mrisho Mpoto y explora más allá de las letras.

    Conoce a Letras Academy

    ¿Enviar a la central de preguntas?

    Tus preguntas podrán ser contestadas por profesores y alumnos de la plataforma.

    Comprende mejor con esta clase:

    0 / 500

    Opciones de selección